http://crdbbank.com/
Friday, September 16, 2016
Thursday, September 15, 2016
BET-Africa
Do your friends like your partner? Steph tries to get Kamie and Kevin to hash things out but things get out of hand when Eny intervenes. Catch the #FinFabulous drama tonight @ 21:50 CAT.
Coca-cola
BREAKING NEWS: Trey Songz ategemewa kupiga show Coke Studio Africa October hii! Vionjo vyote vya msimu wa nne wa Coke Studio Africa hivi hapa http://spr.ly/6187BAstU
Whitedent Tanzania
Gari letu la maonesho wiki hii litakua maeneo yafuatayo. Tafadhali ungana nasi kwa kwenda kujaza fomu katika sehemu hizi husika ili uweze kuwa mmoja wa mshindi wa magari 25 kutoka whitedent. Karibu sana!
Gari no 1 Kinondoni 1 - Mtaa: manzese daraja
Gari no 2 Kinondoni 2 - Mtaa : Ubungo River side
Gari no 4 Ilala - Mtaa : Buguruni Sheli
Gari no 7 Arusha - Mtaa :Kirombelo bus stand
Gari no 10 Zanzibar - Mtaa : Mkunazini Unguja
Gari no 12 Mbeya - Mtaa : kabwe mbeya
Gari no 15 Songea - Mtaa :Machine ya mpunga (manzese)
Gari no 17 Singida - Mtaa :Msifuni Sokoni
Gari no 18 Tabora - Mtaa :Tabora Stand Mpya
Gari no 19 kigoma - Mtaa :Soko la mwanga
Gari no 24 Geita - Mtaa : nyankumbu
Wakumbuka hili shairi
1. Karudi baba mmoja,
toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja,
na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja,
ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli iwafae maishani.
2. Akatamka mgonjwa,
ninaumwa kwelikweli,
Hata kama nikichanjwa,
haitoki homa kali,
Roho naona yachinjwa,
kifo kimenikabili,
Semeni niseme nini,
kiwafae maishani.
3. Yakawatoka kinywani,
maneno yenye akili,
Baba yetu wa thamani,
sisi tunataka mali,
Urithi tunatamani,
mali yetu ya halali,
Sema iko wapi mali,
itufae maishani
4. Baba aliye kufani,
akajibu lile swali,
Ninakufa maskini,
baba yenu sina hali,
Neno moja lishikeni,
kama mnataka mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
5. Wakazidi kumchimba,
baba mwenye homa kali,
Baba yetu watufumba,
hatujui fumbo hili,
akili zetu nyembamba,
hazijajua methali,
Kama tunataka mali,
tutapataje shambani?
6. Kwanza shirikianeni,
nawapa hiyo kauli,
Fanyeni kazi shambani,
mwisho mtapata mali,
haya sasa buriani,
kifo kimeniwasili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
7. Alipokwisha kutaja,
fumbo hili la akili,
Mauti nayo yakaja,
roho ikaacha mwili,
Na watoto kwa umoja,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
8. Fumbo wakatafakari,
watoto wale wawili,
wakakata na shauri,
baada ya siku mbili,
wote wakawa tayari,
pori nene kukabili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
9. Wakazipanda shambani,
mbegu nyingi mbalimbali,
tangu zile za mibuni,
hadi zitupazo wali,
na mvua ikaja chini,
wakaona na dalili,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
10. Shamba wakapalilia,
bila kupata ajali,
Mavuno yakawajia,
wakafaidi ugali,
Wote wakashangilia,
wakakumbuka kauli,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
11. Wakanunua na ng'ombe,
majike kwa mafahali,
wakapata na vikombe,
mashine na baiskeli,
Hawakuitaka pombe,
sababu pombe si mali,
Kama mnataka mali,
mtayapata shambani.
12. Wakaongeza mazao,
na nyumba za matofali,
Pale penye shamba lao,
wakaihubiri mali,
Wakakiweka kibao,
wakaandika kauli...
"KAMA MNATAKA MALI
MTAIPATA SHAMBANI"
Miaka hiyo tuliimba tu kama kujifurahisha wala hatukujua maana yake, leo twatambua nini maana yake, nasisitiza, kama mnataka mali mtaipata shambani
JINS YAKUONDOA WEUSI KWENYE MAKWAPA
Mobile tracking
Detect Any Mobile Number Location Using This This Application for android... simple and easy to download no survery goto : http://ft7.in/Mobile_Number_Tracker
Wednesday, September 14, 2016
WAZIRI MKUU NAE YUMO
Kwa habari zaidi kuhusu waathirika wa tetemeko mwnza
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Mbatia-alilia-misaada-ya-waathirika-tetemeko/1597578-3381514-oke55u/index.html
Sunday, November 4, 2012
MILA NA DESTURI ZA WAPARE
Tuesday, October 23, 2012
MDAHALO WA KUGOMBEA URAISI
MAREKANI: MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA WA URAIS
Nani msema ukweli? Nani amewashawishi wapiga kura vya kutosha kabla ya uchaguzi? Ni Obama au Romney? Wagombea katika uchaguzi mkuu wa Marekani Barack Obama na Mit Romney wametofautiana kuhusu sera ya kigeni,Obama akisema Romney hana uelewa wowote wa sera ya kigeni wakati Romney akisema Obama alikosea katika sera yake ya Mashariki ya kati. Kwamba amesababisha vurugu zaidi tangu aingine mamlakani.
TAMKO LA RAISI!
Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete , amesema serikali haitawavumilia waumin wachache wa madhehebu ya dini wanaotaka kuvuruga amani ya nchi kwa maslahi yao na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote wanaochochea uvunjivu wa amani.
Monday, October 22, 2012
MZOZO WA TANZANIA NA MALAWI
Rais Jakaya Kikwete anataka mahakama ya kimataifa kuhuzu mizozo kutatua mzozo kati ya nchi yake na Malawi
Hali ya wasiwasi inatanda kati ya Malawi na Tanzania kuhusu mzozo wa mpakani ambao umekuwa ukitokota kwa miaka mingi lakini sasa umefika daraja ya juu katika wiki chache zilizopita.
Mzozo unahusu umiliki wa ziwa Malawi ambalo ni la tatu kwa ukubwa barani Afrika na ambalo linapakana na Malawi, Tanzania na Msumbiji.Tangu miaka ya sitini, Tanzania na malawi zimekuwa zikizozana kuhusu umiliki wa ziwa hilo, lakini mzozo huu wa sasa umekuwa mbaya zaidi hasa ikizingatiwa ripoti za kupatikana gesi na mafuta katika ziwa hilo..Msumbiji haijahusika kivyovyote na mzozo huu..
Nini hasa kinazozaniwa?
Fahari ya nchi na maswala ya kujiendeleza kiuchumi kwa Malawi na Tanzania kila mmoja akisimama kidete kusisitiza msimamo wake. Kwa Tanzania, ziwa hilo linajulikana kama Nyasa, wakati nchini Msumbiji inajulikana kama Lago Niassa. Malawi na Tanzania ni koloni za zamani za Uingereza wakati Msumbiji ilikuwa chini ya ukoloni wa Ureno. Uingereza iliichukua Tanzania kutoka kwa Wajerumani baada ya wao kushindwa katika vita vya kwanza vya dunia. Kando na ripoti za kuwepo mafuta na gesi katika ziwa hilo, ziwa lenyewe ni kivutio kikubwa cha watalii. Malawi inasema inashauriana na Msumbiji kuhusiana na uchimbaji wa mafuta katika siku za baadaye ili kuzuia mzozo wa kidiplomasia . Je hii ni mara ya kwanza kwa mzozo huu wa ziwa Malawi kutokea? Hapana. Mapema miaka ya sitini, Malawi ilidai umiliki wa ziwa hilo kwa kuambatana na makubaliano ya mwaka 1890 Heligoland kati ya Uingereza na Ujerumani ambayo yalisema kuwa mpaka kati ya nchi hizo uko upande wa Tanzania. Makubaliano hayo yaliafikiwa na Muungano wa Afrika na Tanzania ikaitikia ingawa shingo upande. Mzozo mpya kati ya nchi hizo ukaripotiwa tena kati ya mwaka 1967 na 1968.
Kisiwa cha Likoma kwenye ziwa Malawi
Nini chanzo cha mzozo huu wa hivi sasa?
Mwezi Septemba mwaka 2011, Malawi ilitoa leseni ya kuchimba mafuta kwa kampuni ya British Surestream Petroleum Limited. Sehemu iliyotolewa kwa uchimbaji wa mafuta ni sehemu yenye mraba wa kilomita 20,000 sehemu ambayo Tanzania inasema ni yake. Vyombo va habari viliripoti mwezi Julai kuwa , mitumbwi ya wavuvi na ya watalii kutoka Malawi inavuka na kuingia upande wa Tanzania Tanzania nayo ikasema kuwa itatafuta ushauri kutoka jamii ya kimataifa ikiwa nchi hizo hazitaweza kusuluhisha mzozo huo zenyewe. Nchi hizo mbili zilifanya mkutano mwezi Julai mjini Dar es Salaam kuhusu mzozo wa mpaka Tarehe 30 mwezi Julai, Tanzania, iliitaka Malawi kusitisha shughuli za kutafuta mafuta kwenye ziwa hilo hadi mzozo kati yao utakaposuluhishwa lakini maafisa wa Malawi wakasisitiza kuwa ziwa hilo lote ni la Malawi na kwamba hakuna sababu ya kusitisha shughuli zake za kutafuta mafuta Tanzania ilisema kuwa ikiwa Malawi itaendelea na shughuli zake kutafuta mafuta itaathiri mazungumzo yanayoendelea kati ya nchi hizo mbili. Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania Bernard Membe alisema kuwa ikiwa Malawi haitafuata maagizo hayo, Tanzania itaiona hatua yake kama kitendo cha uvamizi.
Rais Joyce Banda anataka Muungano wa Afrika kutatua mzozo wa ziwa Malawi
Nini kimesababisha hofu ya hatua za kijeshi?
Hofu ya mzozo kutokota na kuwa mbaya zaidi ilijitokeza wakati Tanzania iliposema kuwa italinda mipaka yake na kuzingatia sheria za kimataifa.Maafisa kutoka pande zote walikutana tena mjini Dar es tarehe 4 na 5 mwezi Agosti, lakini Malawi ilisisitiza kuwa haitasitisha shughuli zake za kutafuta mafuta Waziri wa mambo ya kigeni wa Tanzania Membe alinukuliwa akisema katika taarifa yake kali kuwa watapambana na Malawi kijeshi. Matamshi yake aliyatoa bungeni kulingana na taarifa kwenye mtandao wa The Guardian. Mtandao wa Nyasa Times ulitoa taarifa kuonyesha kuwa kuna taharuki kati ya nchi hizo mbili kuhusu mpaka wa Ziwa , lakini waziri wa usalama wa ndani wa Malawi Uladi Mussa akasisitiza utulivu. "Tunashauriana na serikali ya Tanzania na mambo yatakuwa sawa. Ikiwa hali itakuwa mbaya kesi hii tutaiwasilisha kwa mahakama ya kimataifa ya haki" alisema waziri huyo. Mnamo tarehe 11 mwezi Agosti, Rais wa Malawi Joyce Banda alisema kuwa yuko tayari kufanya kila hali ikiwemo kujitolea maisha yake kwa sababu ya watu wa Malawi. Watanzania wanaoishi karibu na ziwa hilo wakaanza kutoroka wakihofia vita. Je kumekuwa na juhudi za kidiplomasia kumaliza mzozo huu? Maafisa wa chi hizi mbili walikutana kati ya tarahe 20 na 25 mwezi Agosti, mjini Mzuzu,Kaskazini mwa Malawi, lakini Rais Banda akarejelea msimamo wake kuwa ni wazi kuwa Ziwa hilo ni la Malawi. Wakati wa mkutano wa chi za ukanda wa Afrika Kusini (SADC),nchini Msumbiji, Rais Banda alikutana na mwenzake wa Tanzania Jakaya Kikwete, aliyekana kuwa nchi yake inajiandaa kwenda vitani na Malawi. Kikwete alisema kuwa matamshi kuhusu vita yalitolewa na wanasiasa wa upinzani ambao wana jazba. Mjini Mzuzu mkutano uliisha bila maafikano. Siku chache baadye Rais Banda alisema kuwa mzozo huo utasuluhishwa katika mahakama ya kimataifa ya ICJ. Malawi baadaye ilikosa kufika kwenye mkutano kati yake na Tanzania kati ya tarehe 10 na 15 Oktoba kulingana na mtandao wa The Citizen
Ziwa Malawi
Je Juhudi za kidipmomasia zimefanikiwa?
Hapana. Mwanzo Tanzania imepandisha mzozo huo kwenye daraja ya juu zaidi kwa kutoa ramani mpya inayoonyesha mpaka ulio katikati mwa ziwa Nyasa. Afisaa mmoja kutoka wizara ya nyumba wa Tanzania amesema kuwa ramani hiyo inaondoa hali ya kutoelewana kwa kuonyesha mpaka unaozozaniwa. Tarehe tatu mwezi Oktoba Rais Joyce Banda aliakhirisha mkutano kati ya nchi hizo mbili hadi Tanzania itakapojieleza kuhusu ramani hiyo. Alimtuhumu Rais Kikwete kwa kumhadaa na kwamba anapanga kulipua mitumbwi ya Malawi katika ziwa hilo. Kikwete alitangaza siku hiyo hiyo kuwa Tanzania itawasilisha kesi yake katika mahakama ya kimataifa ya mizozo. Kwa upande wake Rais Banda ameutaka muungano wa Afrika kuingilia kati mozo huo. Je mzozo huu ni kuhusu mpaka tu au kuna jengine?
Sunday, October 21, 2012
Duru za jeshi la Guinea Bissau, Afrika Magharibi, zinaeleza kuwa watu waliokuwa na silaha wameuwawa kwenye shambulio dhidi ya kambi ya jeshi nje ya mji mkuu, Bissau.
Inaarifiwa mapambano yaliendelea kwa saa nzima. Waandishi wa habari wanasema shambulio hilo lilofanywa usiku wa manane, litazidisha wasiwasi Guinea Bissau, ambako jeshi lilipindua serikali mwezi wa Aprili. Fujo za mara-kwa-mara nchini Guinea Bissau zimeifanya nchi hiyo kuwa pahala pa kupitisha magendo ya mihadarati, baina ya Amerika Kusini na Ulaya.





